NASH MC NI SAUTI YA MTAA.



NASH MC ni moja kati ya  rapper wanao unda kundi la milaba minne(wachache wanalijua hii) linalo patikana katika kundi mama la TAMADUNI MUZIK ndani ya label kongwe "MUSIC LABORATORY" nash ni moja kati ya rapper wenye misimamo mikali ya mziki, pia nash anatambulika kwa uwezo wake wa uandishi wa mashairi na utumizi fasaha wa  lugha ya kiswahili katika mziki wake

Nash Mc anata umaarufu mkubwa kwenye mziki wa hip hop TANZANIA kwa uwezo wake wakusimamia movement kubwa na zenye changamoto kubwa peke yake na kufanikiwa kwa kiasi kikubwa na mitaa hudhililisha mapenzi yake kwa ku support movement zake na mziki wake kiujumla 


Hili limeonekana hivi karibu pale mashabiki zake walivyo amua kudhihilisha hili mitaa kwa ku print jina la rapper huyo kwenye walls za mitaa na kuonesha kuwa wana mpenda sana nash na wanakubali anachokifanya 

Chapisha Maoni