TRACK OF THE WEEK - NIKK MBISHI ft NURUEL - AU


                             


Pakua Free "Track Of the Week" Nikk Mbishi ft nuruel - Au Mp3, Tangu nisikikilize track zote za nikk mishi sijawahi sikia track ya mapenzi kali kama hii kuanzia mpangilio wa matukio na visa. Kwenye kiitikio kama ilivyo kawaida yake nuruel hajafanya makosa pakua hapa Click Here Na usikilize madini haya.

RAPPER WAKAZI ATEULIWA KUWANIA TUZO ZA KORA KATIKA KIPENGELE CHA "BEST HIP-HOP ACT"

 
tanzania rapper wakazi



Habari njema kwa mashabiki wote wa rapper wakazi, Ni kwamaba siku zote ukifanya kitu kizuri mafanikio ni lazima yatakufata haijalishi eneo ulilopo au aina ya lugha unayotumia kuwakilisha mziki wako. Kwa mara ya kwwanza kwa rapper wakazi ametauliwa kuwani katika tuzo za KORA katika kipengele cha best hip hop act kwa africa.

Rapper wakazi anachuana vikali na rapper wezake wakali kutoka afrika akiwemo rapper kama SARKODIE kutokea GHANA, STANLEY ENOW kutokea CAMEROON, HAMZAOUI MED AMINE kutokea TUNISAI, Kiff No Beat (Cote D'voire) na Rapper KO kutokea SOUTH AFRICA.

Shindano hili la KORA MUSIC AWARD litafanyikia katika mji wa Windhoek Namibia mnamo tarehe 20th 2016, Maswala ya upigaji na njia za kutumia kupiga kula mtafahamiswa . Pia rapper wakazi amefulahisha sana na kitendo hichi cha kuchaguliwa kuwa miongoni mwa marapper watakao shindanishwa katika tuzo hizo za kora music award. Wakogwe wa mziki na harakati za mziki wa hip hop kama ZAVARA na Xsamiasiku4saa4 wamempa bara zote na kumsihi kuwa ushindi wake katika tuzo hizo ni ushindi wa marapper wote wa bongo.

                                      
Pia ikumbukwe kuwa rapper wakazi atakuwa anachuana vikali na rapper wekaze wakali na wakubwa bara afrika, Kwa hiyo swala la kumpigia kula ni swala la muhimu sana ili kufanikisha swala hii na ushindi kwa nchi yetu na fulaha kwa mziki wa bongo pia. Upatapo taarifa hizi mjulishe na mwezako kuwa rapper wakazi anahitaji support yako.

                                        





NEW TRACK COMING SOON 7th December - JAY MOO ft DEDDY "HILI GAME"



J moo - Hili game


Kama ilivyo ada wakubwa na wadongo yule rapper mkongwe na na mahili wa uandishi wa mashairi  katika mziki wa bongo hip hop si mwingine ni "Mjukuu Wa Mchopanga" a.k.a Jay Moo anakuletee track mpya akiwa amemshirikisha deddy,  Kama ni mfatiliaji wa mziki wa bongo hip hop kwa muda mrefu huwezi kubishana na mimi kuwa Jay moo ni moja kati ya rapper siku zote wanaounda list ya rapper bora kumi wa mziki wa hip hop kwa hapa kwetu bongo. Siku zote Jay moo anapoamua kufanya kitu huwa hakosei. Uwezo wa Jay moo kiuandishi ni mkubwa sana kitu kinachofanya watu wengi kuendeleea kumpenda hata kama hana tracks mpya hewani.

Tarehe 7 ya mwezi wa kumi na mbili kaa tayari kwa mziki mzuri na makini kutoka kwa watu makini. Track hii mpya ya Jay moo imefanyika katika studio za BONGO RECORD chini ya usimamizi wa producer P-Fank Majani, Hii nayo ni habari nzuri kwa sisi wafatiliaji wa mziki wa hip hop Jay moo anapo kutana na producer wake wa siku nyingi siku zote hakihalibiki kitu.  Kaa tayari shabiki kwa mziki wa wateule mziki ulioenda shule...........!!!.



HAPPY BIRTHDAY- FREDRICK BUNDALA a.k.a SKY WALKER




Hakika ukitaja kati ya watangazaji walio wahi kukonga nyoyo za wasikilizaji wengi wa redio hususa katika maswala ya kimziki hususa bongo fleva na hip hop Tanzania huwezi kuacha kumtaja Fredrick Bundala a.k.a Sky Walker. Sky kama ilivyo kawaida ya wadau wengi wa mziki hupendelea kumuita siku zote kwa kutumia jina hilo amekuwa mstari wa mbele kutoa mchango wake wa hali na mali kuendeleza na kusupport mziki wa kitanzani toka akiwa kama mtangazaji wa redio katika vipindi mbali mbali vya mziki na kijamii.

Umaarufu wa sky ulianzia tokea akiwa katika redio free africa katika kipindi kama "Extra Show Time" uwezo wake mkubwa wa kuweza kufahamu mziki wa kibongo hata wa kimataifa ulimfanya kuweza kupata urafiki na wasanii wengi wa kubwa hapa ndani na nje ya nchi na kuweza kupata mashavu mbali mbali ya kutengeneza matangazo mbali mbali ya vipindi vya redio.

Kwa sasa sky alipumzika katika mambo ya utangazaji na kuhamia katika mambo ya kimitandao kuweza kupush huu mziki wa kitanzania kupitia social networks mbali mbali. Kwa sasa sky ni moja kati ya wahusika wakuu wa uandishi wa makala mbali mbali katika mtandao wa www.bongo5.com akiwepo na mwezake rafiki yake kipenzi toka enzi hizo za redio free africa George Sandu a.k.a Kid bway

Sisi kama tzhiphopnew tunapenda kutoa salamu zetu za dhati na kheri ya kuzaliwa kwako bwana sky walker na family wako. Mungu awe na wewe kati maisha yako yote. Ameni.