NEW MIX-TAPE FROM WAKAZI COMING SOON



Webiro N Wakazi maarufu kama WAKAZI yupo mbioni kuachia mixtape (Kanda Mseto) yake mpya hivi karibuni
, ni kwa muda mrefu WAKAZI amekuwa akisikika kuwa yupo katika harakati za kuandaa mixtape yake mpya ambayo mpaka sasa haijafahamika itakwenda kwa jina gani, But ni matalajio yangu kuwa itakuwa moja kati ya mix-tape  nzuri maana sina wasiwasi na uwezo wa WAKAZI hasa katika uandaaji wa mixtape kali maana ana uzoefu mkubwa katika uandaji wa album nzuri na kanda mseto na sio mala yake ya kwanza kufanya jambo hii katika ufanisi mkubwa!

Wakazi mpaka sasa ajatamka siku rasimi ambayo ataachia kanda mseto yake  hiyo mpya kwa sababu anasema kuwa kuna baadhi ya mambo bado anayaweka sana na kama yakikaa sawa kama anavyotaka atakuwa hana kipingamizi tena cha kumfanya asiachie kanda mseto hiyo inayo subiliwa kwa shauku kubwa mtaani

Pia kuna uwezekano kuwa wakazi akawa katika mpango pia wa kuachia album yake mpya baada ya kuachia mixtape yake mpya inayo subiliwa na watu wengi mtaani na mimi nikiwa mmoja kati yao. Kama alivyo tamka katika mahojiano ya kipindi cha Ladha3600  kinacho lushwa na redio ya E-fm chini ya utangazaji wa Jabir Saleh , namnukuu;
Nitaachia Mixtape siku za karibuni kabla ya Album kwasababu kuna vitu bado havijakaa sawa
 Hivyo mpaka sasa hatujajua tarehe na siku rasimi ambayo wakazi atatoa mixtape yake ikifatiwa na album yake mpya. Lakini kaa tayari kwa ujio wa kishindo kutoka kwa wakazi. Kinachotakuwa kwako kama shabiki wa kweli ni support yako ya nguvu ili kuweza kufikisha mziki huu wa bongo hip hop mbali zaidi ya hapa ulipo . Pia taarifa hizo utaendelea kuzipata hapa bure kwenye tovuti hii yetu pendwa.

NEW AUDIO: NIKKI MBISHI FT HARD MAN - GOOD VIBES



Download good new music kutoka kwa nikk mbishi ft hard man GOOD VIBES, round hii kwenye nyimbo yake mpya nikki amefanya kitu cha maana na ziada kwa kumshirikisha msanii wa zamani sana na aliye kuwa silent sana kwenye industry ya mziki bila mashabiki zake kujua kipi kilimpata kwa muda wote huu kuwa silent.

Ki-ufupi nyimbo ni nzuri na ina miondoko ya hip hop unaweza pata nakala yako HAPA na kusikiliza na pia kutoa maoni yako kuhusu nyimbo hii, Pia unaweza share na rafiki zako na jamaa ili kuweza kutoa support kwa namna moja au nyingine katika kukuza mziki wa BONGO HIP HOP asante!. 

NEW AUDIO: GOOD MUSIC - BINGO (Boy Stimela) ft EDDY MC

 New bongo hip hop music toka kwa bingo a.k.a Boy Stimela


New bongo hip hop music toka kwa bingo a.k.a Boy Stimela ft Eddy Mc, Moja katika ya wasanii tokea Dar wenye uwezo mzuri wa kuandika na kuflow vizuri haswa linapokuja swala la mziki mzuri katika lugha ya kiswahili. Pia ni moja kati ya rapper walio kwisha fanya mziki toka zamani na rapper maarufu kama STEREO na wengine toka Dar.

Unaweza pata nakala ya nyimbo hiyo HAPA na kuisikiliza kwa umakini na unaweza kunambia kipi umekiona kwa rapper huyu je ?, Anaweza au laa!!

Nyimbo imefanyika chini ya studio ya 99 Records.

NEW VIDEO: MNAZ MC ft CHINDO MAN - I'M PEACE




Mnaz Mc ni moja kati ya wasanii wapya kwenye mziki wa bongo hip hop tokea ARUSHA, Pia nikati ya wasanii waliopo chini ya record label ya WATENGWA RECORD chini ya usimamizi wa chindo man rapper bora na mahiri tokea ARUSHA japo kimaisha mara nyingi yupo abroad

Watu wengi watakuwa hawamfahamu rapper huyu  kutokana na kuwa mgeni masikioni mwa wasikilizaji wa mziki wa bongo HIP HOP wengi, But wait ni kwambie kitu..!!

Je wajua Mnaz MC was winner of African Music Now Freestyle Battle in Kijenge Juu, moja ya sifa inayoweza kukupa ushawishi wakumsikiliza kwa umakini na kumpokea katika mziki wa BONGO HIP HOP ili aweze kukimbiza kijiti kama rapper wengine wakwogwe au wapya katika mziki huu wa bongo hip hop

VIDEO imefanyika chini ya usimamizi wa Africanmusicnow na kuwa filmed and directed by Dony and Davy K of D.I.D. Entertainment. Waweza itazama video hiyo hapa chini na kutoa support yako kwa kushare na watu mbali mbali ili kuweza kufikisha mziki wetu wa bongo hip hop mbali..



NEW AUDIO: SISI - GODZILLA ft STEREO ft ONE THE INCREDIBLE ft NIKK MBISHI

 Godzilla ft One the Incredible ft Stereo ft Nikk Mbishi inayokwenda kwa jina la SISI


Download nyimbo mpya kutoka kwa Godzilla ft One the Incredible ft Stereo ft Nikk Mbishi inayokwenda kwa jina la SISI,  Kama kawaida ujuavyo katika mziki wa HIP HOP  wanapokutana wa kali katika bongo hiphop music huwa kila mtu kwa uwezo wake binafsi kujitahidi kufanya kitu kizuri kwa ajili ya mashabiki wake wake na hapo ndipo mziki mzuri hutokea.

Kila mtua anajua uwezo wa wa saniii hawa ki-uwezo binafsi mmoja baada ya mmoja kwa hiyo kazi kwako kusikiliza nyimbo ki-umanikini na kutuoa mtanzamo wako kipi umependa katika nyimbo zima na kipi hujakiependa

Nyimbo hii umetayarishwa na producerKIBABU WAPOTEEN  chini ya studio ya KILI RECORDS 

Nyimbo unaweza kuipakua HAPA pia na  kushare na wapenda mziki wa hip hop na kutoa support yako katika mziki wa bongo hip hop kwa namna moja au nyingine.


TOP 5 BEST BONGO RAPPER OF ALL TIME

TOP 5 BEST  BONGO RAPPER OF ALL TIME


Okey, ni kwa muda sana nimekuwa nikitaka kuandika kuhusu swala hili ya rapper bora wa siku zote kwetu hapa Tanzania, Lakini nimekuwa sipati muda kutokana na harakati na projects tofauti tofauti za kimaisha. Lakini kwa neema ya Mungu leo nimepata muda na nikaona sio vibaya nikaandika kuhusu swala hili, 

Kabla ya kuandika swala hii napenda kutoa vigezo nilivyotumia kuweza kutengeneza list hii ya rappers watano wakali wa siku zote kutoka hapa kwetu Tanzania ni kama ifuatavyo

  1. Uwezo wa uandishi wa mashairi
  2. Uwezo wa kufikisha Ujumbe kwa hadhira 
  3. Uwezo wa kuhimili maada husika katika nyimbo husika
  4. Uwezo binafsi 
  5. Idadi ya nyimbo bora kutoka kwa msanii husika
Bila kupoteza muda naomba tuanze pamoja kuhesabu list yetu ya Top 5 best bongo rapper of all time 

5. Nikk Mbishi 



Namba tano anasimama Nikk Mbishi a.k.a Dr Unju bin uniq, Yeah najua watu wengi wata jiuliza kwanini nikk na sio rapper fulani. . Na shidwa kujiuliza why Mbishi hujiita Unju wasipate jibu lolote okey sio tabu unaweza soma nakala hii Hapa unaweza pata kitu na kutoa utata huo na kuelewa kiundani uwezo wa NICAS 

Watu wengi wanaweza niuliza why ?, Nikk Mbishi. Jibu ni dogo tu "UWEZO" Nikk ni moja kati ya rapper wenye confidence na kuamini binafsi ni moja kati ya rapper bora, Nikk ni kati ya rapper asiwe pelekeshawa na media wala mtu binafsi, Nikk ni  moja kati ya rapper wenye uwezp wa ku stick kwenye maada hasa pale anapo chana, Moja kati ya nyimbo amabazo nikk alisha wahi fanya na kuwa bora kuwahi tokea ni pamoja na KIJUSI, AU, HISIA, KILA SIKU kama umaweza pata hizo nyimbo na kuzisikiliza japo mara tatu kila siku unaweza kubaliana na mimi 

Pia kitu kilichofanya nikk kuwa katika list hii ni uwezo wake wa kuto choka kutoa ngoma, Washikaji wengi wamekuwa wakisema nikk ni kisima cha mziki hakiwezi kau leo wala kesho, kila siku nikk harakati mwanzo mwisho 

4. Jcb  Makalla 




Ukisikia Paaa!! Ujue imekukosa... Jcb makalla moja kati ya rapper wakali tokea Arusha japo kwa sasa kifamilia yupo aboard. Watu wengi wana weza shangazwa na list hii but kwa wafatiliaji  wa muda mrefu hawawezi bishana na mimi uwezo wa JCB ni mkubwa sana hasa kiuandishi na ku-rap JCB ni moja kati ya rapper pale unapo wapa topic ya kuzungumzia hufanya kitu roho inapenda

JCB ni moja kati ya rapper wenye flow adimu sana kwenye mziki wa bongo tofauti na rapper wa kisasa kila rapper akiflow ni yale yale tu, But hata ukiwa usingizini JCB ni kati ya rapper atakufanya uamke ukiwa usingizini, ukae na usikilize kwa makini na naamini mwisho ya nyimbo lazima upate kitu na utikise kichwa 

Namba nne yetu kwa leo imekwenda kwa JCB rapper mkongwe ma makini toka Arusha 



3. Jay Moo



Jay moo, mzee wa stori tatu tofauti, hit maker wa pesa madafu. Jay moo ni moja ya wasanii wa zamani kwenye mziki wa bongo hip hop, Kutokana na uwezo wake chini ya usimamizi wa producer bora bongo a.k.a father of bongo fleva P-Fank Majani  amekuwa msanii ambaye hutoma nyimbo zale kwa muda na kufanya vizuri

Jay moo ni moja katika ya rapper wanaopatika katika kundi la WATEULE akimemo SOLO THANG, MCHIZ MOX. Sababu kubwa iliyonifanya kuweza kumuweka Jay moo  kwenye hii list ni pamoja na idadi ya hit song zake ambazo alisha kwisha zitoa toka muda mrefu na kuwa bora zilizo andikwa katika ujuzi wa hali ya juu ndani ya msingi ya hip hop na ujumbe katika nyimbo zake zote


2. Fid Q






Fid Q a.k.a Jeshi la mtu mmoja, rapper toka mwanza rapper mwenye uandishi mgumu kuelewa na utunzi wa hali ya juu. Kitu kinacho mtofautisha Fid Q na rapper wengi bongo ni uwezo wa kutumia kiswahili na misamiati migumu kwenye mziki wake, 

Kila mtu anajua uwezo wake katika rapping career, ni moja katika ya rapper wanaoshikilia tuzo ya best male hip hop artist. Fid ni moja kati ya rapper wenye hit song nyingi sana na zenye ujumbe mkali. Wengine humuita fid kuwa ni Nas wa bongo kutokana na uwezo wake wa uandishi na story katika nyimbo zake 


1. Profesa Jay






Mwana msolopa ganzi, wa mitulinga father of bongo rapping career, Pro Jay ni moja kati ya rapper waliofanya mziki huu wa bongo hip hop kufika hapa ulipo kutokana na uwezo wake Pro Jay ameweza ku washawishi wazazi wa rapper wengi wa sasa kuweza kufungua milango kwa watu wengi kuamini kuwa mziki sio uhuni

Pro Jay kwa sasa ni mbunge katika maswala ya kiserikali ni moja kati ya wasanii wenye uwezo mkali wa utunzi wa nyimbo zenye ujumbe mkali na zenye maadili katika jamii

Pro Jay ni rapper walio kaa katika game hili la hip hop kwa muda mrefu sana bila kupotea wa kuteteseka ndio sababu kubwa ililo fanya kuwa katika list hii hasa namba moja pia