NEW MIX-TAPE FROM WAKAZI COMING SOON



Webiro N Wakazi maarufu kama WAKAZI yupo mbioni kuachia mixtape (Kanda Mseto) yake mpya hivi karibuni
, ni kwa muda mrefu WAKAZI amekuwa akisikika kuwa yupo katika harakati za kuandaa mixtape yake mpya ambayo mpaka sasa haijafahamika itakwenda kwa jina gani, But ni matalajio yangu kuwa itakuwa moja kati ya mix-tape  nzuri maana sina wasiwasi na uwezo wa WAKAZI hasa katika uandaaji wa mixtape kali maana ana uzoefu mkubwa katika uandaji wa album nzuri na kanda mseto na sio mala yake ya kwanza kufanya jambo hii katika ufanisi mkubwa!

Wakazi mpaka sasa ajatamka siku rasimi ambayo ataachia kanda mseto yake  hiyo mpya kwa sababu anasema kuwa kuna baadhi ya mambo bado anayaweka sana na kama yakikaa sawa kama anavyotaka atakuwa hana kipingamizi tena cha kumfanya asiachie kanda mseto hiyo inayo subiliwa kwa shauku kubwa mtaani

Pia kuna uwezekano kuwa wakazi akawa katika mpango pia wa kuachia album yake mpya baada ya kuachia mixtape yake mpya inayo subiliwa na watu wengi mtaani na mimi nikiwa mmoja kati yao. Kama alivyo tamka katika mahojiano ya kipindi cha Ladha3600  kinacho lushwa na redio ya E-fm chini ya utangazaji wa Jabir Saleh , namnukuu;
Nitaachia Mixtape siku za karibuni kabla ya Album kwasababu kuna vitu bado havijakaa sawa
 Hivyo mpaka sasa hatujajua tarehe na siku rasimi ambayo wakazi atatoa mixtape yake ikifatiwa na album yake mpya. Lakini kaa tayari kwa ujio wa kishindo kutoka kwa wakazi. Kinachotakuwa kwako kama shabiki wa kweli ni support yako ya nguvu ili kuweza kufikisha mziki huu wa bongo hip hop mbali zaidi ya hapa ulipo . Pia taarifa hizo utaendelea kuzipata hapa bure kwenye tovuti hii yetu pendwa.

Chapisha Maoni