HAPPY BIRTHDAY- FREDRICK BUNDALA a.k.a SKY WALKER




Hakika ukitaja kati ya watangazaji walio wahi kukonga nyoyo za wasikilizaji wengi wa redio hususa katika maswala ya kimziki hususa bongo fleva na hip hop Tanzania huwezi kuacha kumtaja Fredrick Bundala a.k.a Sky Walker. Sky kama ilivyo kawaida ya wadau wengi wa mziki hupendelea kumuita siku zote kwa kutumia jina hilo amekuwa mstari wa mbele kutoa mchango wake wa hali na mali kuendeleza na kusupport mziki wa kitanzani toka akiwa kama mtangazaji wa redio katika vipindi mbali mbali vya mziki na kijamii.

Umaarufu wa sky ulianzia tokea akiwa katika redio free africa katika kipindi kama "Extra Show Time" uwezo wake mkubwa wa kuweza kufahamu mziki wa kibongo hata wa kimataifa ulimfanya kuweza kupata urafiki na wasanii wengi wa kubwa hapa ndani na nje ya nchi na kuweza kupata mashavu mbali mbali ya kutengeneza matangazo mbali mbali ya vipindi vya redio.

Kwa sasa sky alipumzika katika mambo ya utangazaji na kuhamia katika mambo ya kimitandao kuweza kupush huu mziki wa kitanzania kupitia social networks mbali mbali. Kwa sasa sky ni moja kati ya wahusika wakuu wa uandishi wa makala mbali mbali katika mtandao wa www.bongo5.com akiwepo na mwezake rafiki yake kipenzi toka enzi hizo za redio free africa George Sandu a.k.a Kid bway

Sisi kama tzhiphopnew tunapenda kutoa salamu zetu za dhati na kheri ya kuzaliwa kwako bwana sky walker na family wako. Mungu awe na wewe kati maisha yako yote. Ameni.

Chapisha Maoni